Skip to main content

Mkuki na Nyota Publishers

Kusadikika

No reviews yet
Product Code: 9789976973105
ISBN13: 9789976973105
Condition: New
$30.78

Kusadikika

$30.78
 

Kwa zaidi ya miaka kumi na tano vitabu vya mwandishi maarufu kushinda wote katika jamii za Waswahili kote Afrika ya Mashariki na Kati, Marehemu Sheikh Shaaban Robert, havikupatikana Tanzania. Sababu ya kukosekana kwa vitabu hivyo ni kuwa kampuni ya kigeni iliyovichapisha iliamua kuacha kuvichapisha kwa sababu haikulipwa kwa fedha za kigeni jambo, lililosabishwa na hali mbaya ya uchumi. Athari za kupotea kwa vitabu vya Sheikh Shaaban Robert katika miaka hiyo ni kwamba Watanzania wengi hasa wale wenye umri chini ya miaka thelathini, hawamjui mwandishi huyu maarufu na hawakulelewa katika mazingira ya utajiri wa maandishi yake ambayo bila shaka yoyote ni mfano pekee wa utajiri wa urithi wa utamaduni wetu. Kwa kuvichapisha vitabu vya Marehemeu Sheikh Shaaban Robert tunawakaribisha tena Watanzania, hasa vijana kuvisoma, kuburudishwa na kufunzwa na yale aliyoyaandika kwa sanaa na kipaji adimu.

First published at the height of colonial occupation, this is an allegorical work of an imaginary country or state in which injustices are perpetrated against all notions of justice, law and humanity. From the master of Swahili language and culture.




Author: Shaaban Robert
Publisher: Mkuki na Nyota Publishers
Publication Date: Dec 12, 1991
Number of Pages: 72 pages
Binding: Paperback or Softback
ISBN-10: 9976973101
ISBN-13: 9789976973105
 

Customer Reviews

This product hasn't received any reviews yet. Be the first to review this product!

Faster Shipping

Delivery in 3-8 days

Easy Returns

14 days returns

Discount upto 30%

Monthly discount on books

Outstanding Customer Service

Support 24 hours a day